Baada
ya hapo alijihisi kama anajivua toka katika mwili, mithili ya nyoka
anayejivua gamba. Ghafla akawa kama anazama katika giza kubwa na
macho yake yakififia mithili ya taa hafifu katika ukungumzito.
Sambamba na hilo alianza kuhisi joto likiongezeka na kuwa kali na
harufu mbaya ya moshi wa yai lililooza ukiibuka. Kwa sabau alikuwa
mtaalam wa kemia, Jabu alijua ni salfa inayoungua. Hakuweza kupumua
vizuri kabisa kwa moshi mzito na harufu kali. Hofu kuu ilimshika, na
hakuelewa ch kufanya. Kufumba na kufumbua, Jabu alikuwa katika eneo
kubwa ambalo hakuweza kujua limeanzia wapi wala kuishia wapi.
Alichoona ni moshi mzito na giza nene. Alichosikia ni sauti nyingi
sana zikilia kwa maumivu makali. Hakujua kama alikuwa analia au
anagugumia, lakini alijua kwa hakika alikuwa akisaga meno kwa maumivu
makali aliyoyasikia.
Jabu
alikumbuka siku moja kanisani ambapo mchungaji wake elielezea sehemu
inayoitwa kuzimu, ambayo inafanana na hapa alipo. “hapana, sio
kwamba panafanana, ndio penyewe!” alijisemea moyoni. Jabu alianza
kujilaumu kwa nafasi zote alizozipoteza. Akakumbuka watu waliomsihi
kwa machozi na kumwonyesha njia impasayo, lakini aliwadharau na
kuwapuuza. Sasa alikuwa katika mahali alipodhani hapakuwahi kuwepo,
na alijua hakuna jinsi ya yeye kutoka. Alitamani iwe ndoto, lakini
haikuwa hivyo.
Aliwashukuru
wale watu walioonekana vichaa njiani wakidharauliwa,kwa upendo wao.
Moyo wake ulimuuma sana. Akamkumbua rafiki yae Mwema, aliyekuwa
akienda kanisani kila siku na hakuchukua muda kumuonya. “Pengine
angesema kwa kuwa ni rafiki yangu ningemsikia”. Namchukia kwa
alilolifanya. Alitamani arudi akawonye rafiki zake kuwa kuzimu ipo,
na sio mahali pa kwenda, lakini hakuwa na namna. Kifo kilikuwa
kimemtenga na mahali pa walio hai, tumaini na wema vimemwacha.
Aliungana na aliowakuta huko kulia kilio cha kukata tamaa......!
Kuzimu na Jehanamu Ipo
Watu
wengi wanadhani hii ni hadithi ya kufurahisha kama ilivyo hekaya za
abunuwasi au alfu lela-ulela. Shetani, adui wa roho yako anajua pia
kama ataifanya Jehanamu na Ziwa la mot vionekane ni visasili,
atakufanya uvipuuze. Lakini hebu jiulize: unawekeza nguvu na
raslimali zako kiasi gani kuhakikisha unaishi maisha mazuri hapa
duniani? Umesoma vitabu vingapi vya “jinsi ya kufanikiwa” au
vifananvyo na hivyo? Mara ngapi umefanya hili na lile kuhakikisha
unafanikiwa? Au ni miaka mingapi umekuwa shuleni lengo likiwa ni
ufanikiwe? Halafu jiulize umetumia raslimali kiasi gani kujua
utakakokwenda baada ya miaka michache sana uliyo nayo? Utagundua
unatania!
Neno
la Mungu lipo wazi kuwa baada ya kifo ni hukumu (Waeb 9:27). Ukifa
faili la maisha yako linakuwa limefungwa na mahali pa kwenda
pameamuliwa. Mungu aliyeumba mbingu na nchi, aliweka utaratibu wa
sisi kuishi katika dunia yake (Kutoka 20:3-17). Alikataza watu kusema
uongo, kuiba, kuwa na miungu, katika dunia yake. Na aliweka adhabu
kwa wavunjaji wote, nayo ni Ziwa la moto (Ufun 21:8, 1 Kor
6:9). Baada ya kufa nafsi yako
itakwenda “selo” kusubiri siku ya kusomewa hukumu yako. Huko
ndiko kuzimu ambako hakuna raha bali ni maumivu (Luke
16:22-24). Utakuwa ukijielewa na maumivu utayasikia. Hili ni tone tu
ukilinganisha na hukumu yenyewe.
Neno liko wazi kabisa
kuwa iko siku Mungu ameiandaa kwa ushahidi kabisa (tazama somo
hili kwa makala inayohusiha hilo). Wengi wanadhani Mungu ni kama
mjomba Santa, akileta zawadi za Krismasi. Lakini kwa kweli wengi
watapigwa namshangao watakapokutana uso kwa uso na Muumba wao. Mungu
anatisha kwa kuwa ni mkuu mno. Yeye Mungu “ambaye yeye peke yake
hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala
hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. ” (1Tim 6:16).
Mpendwa wangu, Mungu sio yule uliyedanganywa. Na kwa hasira yake
aliiandaa Jehanamu ya moto kwa shetani na wote watakaomfuata katika
uasi wa sheria ya Mungu.
Baada ya Mungu wa haki
kukuonyesha yote uliyofanya na jinsi bila soni ulivyovunja amri zake
atakuhukumu kwenda katika ziwa la moto. Wewe na selo mtatupwa katika
gereza la mwisho, yaani Ziwa la moto (Ufun 20:14-15). Hapo ni kilio
na kusaga meno milele maana huko “funza wao hafi, wala moto
hauzimiki” (Mark 9:46, Luk 13:28).
Jehanamu siyo sehemu ya
kwenda mpendwa, na Mungu siyo wa kukutana naye kama jaji, maana
anatisha. Yesu mwenyewe alionya kuwa kama “mguu wako ukikukosesha,
ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na
miguu miwili, na kutupwa katika jehanum” (Mark 9:45). Jehanamu ni
mahali pabaya kiasi kwamba nakushauri kama gari lako, mke, mume au
chochote kitakuwa sababu ya wewe kwenda huko kitupe.
Yawezekana umeashaanza
“kutenda mema” ili upate sababu ya Mungu kukuruhusu uende
mbinguni. Nikuhakikishie hata utende mema kiasi gani hayafuti makosa
uliyofanya, na kujaribu kumhonga Mungu matendo yako ili “asahau”
makosa yako ni kosa kubwa zaidi. Mungu anayaita matendo yako hayo
kuwa ni kama “nguo iliyotiwa unajisi” (Isay 64:6). Usijaribu
kumpa Mungu rushwa ya matendo mema, hataipokea! Na usijidanganye
kwamba Mungu atakusamehe”ukitubu”. Jaribu kumwambia hakimu
nimeiba ila ninatubu, nisamehe uone. Kama mwanadamu anasimamia sheria
za wanadamu vema, unadhani Mungu si zaidi kusimamia sheria zake
mwenyewe?
Waweza kuwa unajiuliza
kuwa “kama ni hivyo nifanye nini sasa ili nami niiepuke Jehanamu?”
Jibu ni kuwa huna cha kufanya. Mungu alifanya mwenyewe. Mungu
alitwaa mwili akakaa kwetu (Yoh 1:14) akaishi maisha matakatifu na
kufa kwa ajili yetu, akilipa deni la hatia yetu: ili sisi tulio wa
dhambi na tuliohukumiwa Jehanamu tupate kwenda Mbinguni. Yesu alilipa
deni la dhambi zote hivyo hakuna sababu ya wewe kwenda Jehanamu.
Unachopaswa kufanya ili deni la uasi wako lifutwe ni kumkiri Yesu kwa
kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa
alikufa kwa makosa yako na kuomba akusamehe na kukuosha dhambi zako,
utaokoka!
Pamoja na kuwa Mungu
amelipa, kuna watu watakwenda huko kwa sababu ya kiburi. Ukikataa
neema ya Mungu leo utajutia siku moja. Na siku hiyo yaweza kuwa hata
leo. Je wajua kitakachofuata dakika tatu zijazo? Usiwe mpumbavu kama
Jabu, kupoteza nafasi hii adimu.mkiri Yesu leo akuokoe na adhabu kali
ya Mungu wa Mbinguni.
Bwana Yesu na akubariki,
Maranatha!