Tuesday, May 20, 2014

Siku Utakapovuta Pumzi yako ya Mwisho

Jabu alikuwa anatembea barabarani kwenda kumwona mkewe. Mkewe alikuwa na malaria na alikuwa amepumzishwa katika zahanati ya mtaa wao. Akiwa anavuka barabara ya mwisho kabla ya kuifikia zahanati, ghafla anasikia watu wakipiga kelele za uoga. Alipogeuka akaona lori la mizigo limeacha barabara likimfuata. “mamaaa!” akapiga kelele ukijaribu kulikwepa. Kitu cha mwisho anachokumbuka ni kishindo kikubwa na maumivu makali.

Baada ya hapo alijihisi kama anajivua toka katika mwili, mithili ya nyoka anayejivua gamba. Ghafla akawa kama anazama katika giza kubwa na macho yake yakififia mithili ya taa hafifu katika ukungumzito. Sambamba na hilo alianza kuhisi joto likiongezeka na kuwa kali na harufu mbaya ya moshi wa yai lililooza ukiibuka. Kwa sabau alikuwa mtaalam wa kemia, Jabu alijua ni salfa inayoungua. Hakuweza kupumua vizuri kabisa kwa moshi mzito na harufu kali. Hofu kuu ilimshika, na hakuelewa ch kufanya. Kufumba na kufumbua, Jabu alikuwa katika eneo kubwa ambalo hakuweza kujua limeanzia wapi wala kuishia wapi. Alichoona ni moshi mzito na giza nene. Alichosikia ni sauti nyingi sana zikilia kwa maumivu makali. Hakujua kama alikuwa analia au anagugumia, lakini alijua kwa hakika alikuwa akisaga meno kwa maumivu makali aliyoyasikia.

Jabu alikumbuka siku moja kanisani ambapo mchungaji wake elielezea sehemu inayoitwa kuzimu, ambayo inafanana na hapa alipo. “hapana, sio kwamba panafanana, ndio penyewe!” alijisemea moyoni. Jabu alianza kujilaumu kwa nafasi zote alizozipoteza. Akakumbuka watu waliomsihi kwa machozi na kumwonyesha njia impasayo, lakini aliwadharau na kuwapuuza. Sasa alikuwa katika mahali alipodhani hapakuwahi kuwepo, na alijua hakuna jinsi ya yeye kutoka. Alitamani iwe ndoto, lakini haikuwa hivyo.

Aliwashukuru wale watu walioonekana vichaa njiani wakidharauliwa,kwa upendo wao. Moyo wake ulimuuma sana. Akamkumbua rafiki yae Mwema, aliyekuwa akienda kanisani kila siku na hakuchukua muda kumuonya. “Pengine angesema kwa kuwa ni rafiki yangu ningemsikia”. Namchukia kwa alilolifanya. Alitamani arudi akawonye rafiki zake kuwa kuzimu ipo, na sio mahali pa kwenda, lakini hakuwa na namna. Kifo kilikuwa kimemtenga na mahali pa walio hai, tumaini na wema vimemwacha. Aliungana na aliowakuta huko kulia kilio cha kukata tamaa......!

Kuzimu na Jehanamu Ipo
Watu wengi wanadhani hii ni hadithi ya kufurahisha kama ilivyo hekaya za abunuwasi au alfu lela-ulela. Shetani, adui wa roho yako anajua pia kama ataifanya Jehanamu na Ziwa la mot vionekane ni visasili, atakufanya uvipuuze. Lakini hebu jiulize: unawekeza nguvu na raslimali zako kiasi gani kuhakikisha unaishi maisha mazuri hapa duniani? Umesoma vitabu vingapi vya “jinsi ya kufanikiwa” au vifananvyo na hivyo? Mara ngapi umefanya hili na lile kuhakikisha unafanikiwa? Au ni miaka mingapi umekuwa shuleni lengo likiwa ni ufanikiwe? Halafu jiulize umetumia raslimali kiasi gani kujua utakakokwenda baada ya miaka michache sana uliyo nayo? Utagundua unatania!

Neno la Mungu lipo wazi kuwa baada ya kifo ni hukumu (Waeb 9:27). Ukifa faili la maisha yako linakuwa limefungwa na mahali pa kwenda pameamuliwa. Mungu aliyeumba mbingu na nchi, aliweka utaratibu wa sisi kuishi katika dunia yake (Kutoka 20:3-17). Alikataza watu kusema uongo, kuiba, kuwa na miungu, katika dunia yake. Na aliweka adhabu kwa wavunjaji wote, nayo ni Ziwa la moto (Ufun 21:8, 1 Kor 6:9). Baada ya kufa nafsi yako itakwenda “selo” kusubiri siku ya kusomewa hukumu yako. Huko ndiko kuzimu ambako hakuna raha bali ni maumivu (Luke 16:22-24). Utakuwa ukijielewa na maumivu utayasikia. Hili ni tone tu ukilinganisha na hukumu yenyewe.

Neno liko wazi kabisa kuwa iko siku Mungu ameiandaa kwa ushahidi kabisa (tazama somo hili kwa makala inayohusiha hilo). Wengi wanadhani Mungu ni kama mjomba Santa, akileta zawadi za Krismasi. Lakini kwa kweli wengi watapigwa namshangao watakapokutana uso kwa uso na Muumba wao. Mungu anatisha kwa kuwa ni mkuu mno. Yeye Mungu “ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. ” (1Tim 6:16). Mpendwa wangu, Mungu sio yule uliyedanganywa. Na kwa hasira yake aliiandaa Jehanamu ya moto kwa shetani na wote watakaomfuata katika uasi wa sheria ya Mungu.

Baada ya Mungu wa haki kukuonyesha yote uliyofanya na jinsi bila soni ulivyovunja amri zake atakuhukumu kwenda katika ziwa la moto. Wewe na selo mtatupwa katika gereza la mwisho, yaani Ziwa la moto (Ufun 20:14-15). Hapo ni kilio na kusaga meno milele maana huko “funza wao hafi, wala moto hauzimiki” (Mark 9:46, Luk 13:28).

Jehanamu siyo sehemu ya kwenda mpendwa, na Mungu siyo wa kukutana naye kama jaji, maana anatisha. Yesu mwenyewe alionya kuwa kama “mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum” (Mark 9:45). Jehanamu ni mahali pabaya kiasi kwamba nakushauri kama gari lako, mke, mume au chochote kitakuwa sababu ya wewe kwenda huko kitupe.

Yawezekana umeashaanza “kutenda mema” ili upate sababu ya Mungu kukuruhusu uende mbinguni. Nikuhakikishie hata utende mema kiasi gani hayafuti makosa uliyofanya, na kujaribu kumhonga Mungu matendo yako ili “asahau” makosa yako ni kosa kubwa zaidi. Mungu anayaita matendo yako hayo kuwa ni kama “nguo iliyotiwa unajisi” (Isay 64:6). Usijaribu kumpa Mungu rushwa ya matendo mema, hataipokea! Na usijidanganye kwamba Mungu atakusamehe”ukitubu”. Jaribu kumwambia hakimu nimeiba ila ninatubu, nisamehe uone. Kama mwanadamu anasimamia sheria za wanadamu vema, unadhani Mungu si zaidi kusimamia sheria zake mwenyewe?

Waweza kuwa unajiuliza kuwa “kama ni hivyo nifanye nini sasa ili nami niiepuke Jehanamu?” Jibu ni kuwa huna cha kufanya. Mungu alifanya mwenyewe. Mungu alitwaa mwili akakaa kwetu (Yoh 1:14) akaishi maisha matakatifu na kufa kwa ajili yetu, akilipa deni la hatia yetu: ili sisi tulio wa dhambi na tuliohukumiwa Jehanamu tupate kwenda Mbinguni. Yesu alilipa deni la dhambi zote hivyo hakuna sababu ya wewe kwenda Jehanamu. Unachopaswa kufanya ili deni la uasi wako lifutwe ni kumkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa alikufa kwa makosa yako na kuomba akusamehe na kukuosha dhambi zako, utaokoka!

Pamoja na kuwa Mungu amelipa, kuna watu watakwenda huko kwa sababu ya kiburi. Ukikataa neema ya Mungu leo utajutia siku moja. Na siku hiyo yaweza kuwa hata leo. Je wajua kitakachofuata dakika tatu zijazo? Usiwe mpumbavu kama Jabu, kupoteza nafasi hii adimu.mkiri Yesu leo akuokoe na adhabu kali ya Mungu wa Mbinguni.

Bwana Yesu na akubariki,
Maranatha!

No comments:

Post a Comment